UGUNDUZI:DAWA YA FANGASI YATHIBITIKA KUVIMALIZA KABISA VIRUSI VYA UKIMWI | Maisha Ni Afya
Breaking News
Loading...

Monday, January 20, 2014

UGUNDUZI:DAWA YA FANGASI YATHIBITIKA KUVIMALIZA KABISA VIRUSI VYA UKIMWI

[2 MB] BONYEZA HAPO CHINI KUPATA MICHONGO MIPYA YA AJIRA DAILY>>>>>>>>> !


Utafiti wa hivi karibuni unaonesha kwamba, dawa ya kupaka ya kutibu fangasi iitwayo Ciclopirox imeweza kupambana na kutokomeza kabisa virusi vya ukimwi vilivyokuwa vimepandikizwa kwenye mchanganyiko maalum wa kimaabara(culture).Cha kufurahisha zaidi ni kwamba,baada ya dawa hiyo kuondolewa kwenye mchanganyiko huo,virusi vya ukimwi havikurudi tena.Vilitokomezwa kabisa.
   Utafiti pia umegundua kwamba,dawa nyingine ambayo hutumika kupunguza madini chuma mwilini iitwayo Deferiprone,nayo pia inaweza kupambana na kutokomeza kabisa virusi vya ukimwi kwenye mchanganyiko maalum wa kimaabara uliokuwa umepandikizwa virusi vya ukimwi.Napo baada ya dawa kusitishwa virusi vya ukimwi havikuweza kurudi tena kwenye mchanganyiko huo.
   Kumbuka kuwa dawa za sasa za kurefusha maisha kwa waathirika wa ukimwi hazina uwezo wa kutokomeza kabisa virusi hivyo na mgonjwa anapositisha dozi virusi hivyo huzaliana tena.
   Watafiti hao kutoka chuo cha tiba cha New Jersey cha nchini marekani waliandika utafiti wao kwenye jarida la PLOS ONE.
   Dawa hizi mbili tayari zinatumika kwa matumizi ya binadamu(japo si kwa kutibu ukimwi),hivyo kuziendeleza mpaka zitibu ukimwi inasemekana kutatumia bajeti ndogo na muda mfupi.
  Daferiprone yenyewe kwa kuwa ni ya kunywa,imejithibitisha kuwa ni salama ndani ya mwili wa binadamu hivyo majaribio ya dawa hii katika kutibu ukimwi tayari yameanza moja kwa moja kwa binadanu bila kupitia hatua ya awali ya kujaribu kwa wanyama.Majaribio hayo yanafanyika nchini afrika kusini.
Chanzo cha habari:www.medicalnewstoday.com
[2 MB] BONYEZA HAPO CHINI KUONA NAFASI MPYA ZA KAZI KILA ZINAPOTOKA>>>>>>>>> !

google+

linkedin

MASWAYETU EXCLUSIVE BLOG
  • Karibu katika Mtandao Huu unaotoa Habari Za Uhakika Kutoka Ndani Na Nje Na Tanzania. Kama una Tangazo,Habari,Picha,Ushauri n.k Wasiliana nasi kwa simu namba 0768 260834. Soma Zaidi

    0 comments:

    POST A COMMENT

     

    IDADI YA WASOMAJI