HAYA NDIYO MADHARA YA KUCHANGANYA POMBE NA DAWA | Maisha Ni Afya
Breaking News
Loading...

Sunday, March 23, 2014

HAYA NDIYO MADHARA YA KUCHANGANYA POMBE NA DAWA

[2 MB] BONYEZA HAPO CHINI KUPATA MICHONGO MIPYA YA AJIRA DAILY>>>>>>>>> !
Pombe ina muingiliano wa moja kwa moja na dawa nyingi tunazotumia.Muingiliano huo huonekana pale pombe na dawa vinapotumika kwa wakati mmoja.Madhara yatokanayo na kuchanganya dawa na pombe yanaweza kuwa madogo yanayovumilika au makubwa yanayoweza kusababisha kifo.Baadhi ya dalili zinazoweza kujitokeza baada ya kutumia dawa na pombe kwa wakati mmoja ni pamoja na kichefuchefu,kichwa kuuma,kutapika,kizunguzungu,kuzimia na mabadiliko ya mzunguko wa damu.Pia kuna madhara makubwa zaidi ambayo ni kuharibika kwa ini,matatizo ya moyo,kutokwa na damu ndani kwa ndani ya mwili na kushindwa kuhema.
Kutumia dawa na pombe wakati mmoja kunaweza kusababisha dawa uliyokunywa au kumeza ipungukiwe ufanisi wake au ishindwe kabisa kufanya kazi.Vile vile dawa na pombe vinaweza kutengeneza sumu hatari mwilini.
Mfano mzuri ni FLAGYL(flajili) dawa inayotumiwa kiholela na wengi kutibu kuharisha,flagyl kama itamezwa pamoja na pombe ndani ya dakika tano yafutayo humpata mtumiaji,presha ya damu hushuka,jasho jingi hutoka,kushindwa kupumua ,kifua kuuma na maumivu ya kichwa,kichefuchefu na kutapika.Ndani ya masaa machache mabaya zaidi hutokea,kifafa na mzunguko wa damu kusimama,hatimaye kifo hutokea kama hakutakuwa na juhudi zozote za kuokoa maisha.
Ulevi kwa upande mwingine unaweza kukufanya usahau kufuata dozi yako hivyo kuharibu tiba.Dawa zenye muingiliano na pombe ni nyingi mno kuzitaja moja moja,kama unaweza,epuka kutumia pombe ukiwa kwenye dozi au wasiliana daktari aliyekuandikia dawa kuhusu muingiliano wa dawa hiyo na pombe.




[2 MB] BONYEZA HAPO CHINI KUONA NAFASI MPYA ZA KAZI KILA ZINAPOTOKA>>>>>>>>> !

google+

linkedin

MASWAYETU EXCLUSIVE BLOG
  • Karibu katika Mtandao Huu unaotoa Habari Za Uhakika Kutoka Ndani Na Nje Na Tanzania. Kama una Tangazo,Habari,Picha,Ushauri n.k Wasiliana nasi kwa simu namba 0768 260834. Soma Zaidi

    0 comments:

    POST A COMMENT

     

    IDADI YA WASOMAJI